Friday, June 22, 2012

KENNETH ASAMOAH ATEMWA YANGA- KLABU KUMLIPA FIDIA

Hatimaye mshambuliaji wa Yanga kutoka Ghana Kenneth Asamoah ametemwa na klabu hiyo baada ya kuitumikia kwa takribani msimu mmoja tu.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka ndani ya Yanga, Asamoah amefikia makubaliano na Yanga kwa kulipwa fidia ya kuvunjiwa mkataba wake aliousaini msimu uliopita.

Kenneth Asamoah anaondoka Yanga huku akiwaachia wapenzi wa klabu hiyo kumbukumbu ya goli zuri la kichwa alilowafunga Simba kwenye fainali ya kombe la Kagame mwaka jana kwenye uwanja wa Taifa.

TIMU 20 KUCHEZA LIGI DARAJA LA KWANZA

Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imeridhia mapendekezo ya Kamati ya Mashindano ya kutaka Ligi Daraja la Kwanza (FDL) kuwa na timu 20 badala ya 18 za sasa.

Lengo la mabadiliko hayo ni Ligi ya Taifa (NL) kuchezwa kwa kanda, hivyo msimu huu timu mbili zaidi (ukiondoa tatu ambazo zimeshapanda kutoka NL) zitaongezwa ili kufikisha idadi ya timu 20 katika FDL.

Timu ambazo zimepanda kutoka NL iliyochezwa katika vituo vitatu ni; Kanembwa JKT ya Kigoma iliyoongoza Kituo cha Kigoma, Ndanda SC ya Mtwara iliyoibuka kinara Kituo cha Mtwara na Polisi Mara iliyokamata usukani katika Kituo cha Musoma.

Kamati ya Utendaji pia imepitisha mapendekezo ya kuchezwa play off ili kupata timu mbili zaidi za kucheza FDL msimu huu. Timu zitakazocheza play off katika utaratibu utakaotangazwa baadaye na Kamati ya Mashindano ni tatu zilizoshuka kutoka FDL na tatu nyingine zilizoshika nafasi za pili katika NL kutoka vituo vya Kigoma, Mtwara na Musoma.

Timu tatu zilizoshuka FDL ni AFC ya Arusha, Samaria ya Singida na Temeke United ya Dar es Salaam wakati zilizoshika nafasi za pili katika NL na vituo vyao kwenye mabano ni Kurugenzi ya Iringa (Mtwara), Mwadui ya Shinyanga (Kigoma) na Tessema ya Dar es Salaam (Musoma).

Hata hivyo, timu zitakazoshuka kutoka Ligi Kuu bado zitaendelea kuwa tatu kama ilivyo kwa zitakazopandwa

AWAMA YA KWANZA USAJILI MWISHO AUGOST 10

Kipindi cha kwanza cha usajili wa wachezaji kwa ajili ya msimu wa 2012/2013 kitamalizika Agosti 10 mwaka huu kulingana na kalenda ya Matukio ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) ya 2012/2013.
Uhamisho wa wachezaji unafanyika kuanzia Juni 15 hadi Julai 30 mwaka huu wakati kipindi cha kuacha wachezaji (sio wa Ligi Kuu. Wachezaji wa Ligi Kuu wanacheza kwa mikataba) ni kuanzia Juni 15- 30 mwaka huu.

Kwa klabu za Ligi Kuu kutangaza wachezaji watakaositishiwa mikataba yao ni kuanzia Juni 15-30 mwaka huu na usajili wa wachezaji unafanyika kuanzia Juni 15 hadi Agosti 10 mwaka huu.

Tunasisitiza kipindi cha usajili kiheshimiwe na mikoa yote kwa sababu usajili huo huo ndiyo utakaotumika katika michuano ya Kombe la FA. Kwa maana nyingine hakutakuwa na kipindi kingine cha usajili wa wachezaji kwa klabu zote nchini hadi hapo litakapofunguliwa dirisha dogo.

Mechi ya kufungua msimu ya Ngao ya Jamii (Community Shield) kati ya mabingwa wa Ligi Kuu, timu ya Simba na makamu bingwa Azam itachezwa Agosti 25 mwaka huu wakati Ligi Kuu itaanza Septemba Mosi mwaka huu, na Ligi Daraja la Kwanza (FDL) yenyewe itaanza Septemba 15 mwaka huu.

Ratiba ya Ligi Kuu itatolewa Julai 23 mwaka huu.

MISRI YAOMBA KUIKABILI NGORONGORO HEROES

Chama cha Mpira wa Miguu Misri (EFA) kimeomba mechi mbili za kirafiki kwa timu yao ya vijana na timu ya vijana wenye umri chini ya miaka 20 ya Tanzania (Ngorongoro Heroes).

EFA imeomba mechi hizo zichezwe Julai 3 na Julai 5 mwaka huu kwa masharti maalumu. Ikiwa zitachezwa Misri, mwenyeji (EFA) atagharamia Ngorongoro Heroes kwa malazi, chakula, usafiri wa ndani na sehemu ya kufanyia mazoezi.

Ikiwa mechi hizo zitachezwa Dar es Salaam, Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) litaigharamia timu ya Misri kwa malazi, chakula, usafiri wa ndani na sehemu ya mazoezi. Hivyo kila timu itajigharamia kwa usafiri wa ndege na posho kwa timu yake.

Sekretarieti ya TFF inafanya uchambuzi wa gharama ili kujua ipi ni nafuu kabla ya kufanya uamuzi wa wapi mechi hizo zichezwe.

Ngorongoro Heroes imeingia raundi ya pili ya michuano ya Afrika ambayo fainali zake zitafanyika mwakani nchini Algeria baada ya kuitoa Sudan katika raundi ya kwanza.

Itacheza mechi ya kwanza ya raundi ya pili Julai 28 mwaka huu jijini Dar es Salaam wakati ya marudiano itakuwa Agosti 11 mwaka huu nchini Nigeria

Friday, May 25, 2012

SHIJI KAGAWA: KUTOKA LIGI YA PILI YA JAPAN MPAKA DORTMOND-SHIJI KAGAWA SUPERSTAR ANAYEFUATIA NDANI YA MAN UNITED.

 

Wakati taarifa za usajili wake kwenda Manchester United zikizidi kukaribia kuwa ukweli, ebu leo tuangalie uchambuzi wa kisoka kuhusu Shinji Kagawa.

Misimu miwil iliyopita, Shinji Kagawa alikuwa hajulikani kabisa nje ya Japan, lakini watu wale wenye macho yanayoona mbali waliona kiungo aliyebarikiwa uwezo wa kucheza soka huku akiisadia klabu yake ya Cerezo Osaka kupanda daraja la juu kwenye soka la Japan ndani ya misimu mitatu tu. Sasa yupo karibuni kujiunga na mabingwa kihistoria wa Barclays Premier league pale Theatre of Dreams - baada ya Red Devils kutuma ofa ya £13miilion kwa Dortmund.

Kagawa alikuwa ndio mjapan wa kwanza kuisaini mkataba wa level ya proffessional kabla ya kumaliza kutoka kwenye elimu ya juu ya sekondari. Akiwa na miaka 18 aliweza kupata nafasi ya kwenye kikosi cha kwanza cha Cerezo, na kujiamini kwake kukapanda sana baada ya kuwa na rekodi nzuri ya kufunga. Kagawa alifunga mabao 27 katika mechi 44 kwenye msimu wa 2009 na kuwasaidia Cerezo kurudi kwenye ligi kuu ya Japan baada ya kushuka kwa miaka 3. Lakini hakuweza kucheza sana kwenye ligi kuu ya Japan, baada ya wakala wa kijerumani Thomas Kroth kushughulikia uhamisho  ambao ulimuamisha kinda hilo kwenda Borussia Dortmnund - wakati timu hilipokuwa ikijipanga upya baada ya kumaliza ligi kwenye nafasi ya 5.

Performance yake pale Dortmund inajieleza yenyewe; kwenye msimu wa kwanza barani ulaya, Kagawa alikuwemo kikosi bora ya Bundesiliga japokuwa alitumia nusu ya msimu kuwa nje ya dimba kutokana  na majeruhi. Mwaka huu, ameweka rekodi mpya kwa Wajapan waliowahi kucheza Ulaya kwa kufunga mabao 13 kwenye mechi 32. Shinji ni hatari kila anapogusa mpira, ana uwezo wa kutengeneza nafasi kwa kutoa pasi za mwisho huku akiwa na uwezo mkubwa wa kupiga mashuti ya mbali.


Nchini kwao Japan, Kagawa ni moja ya wanasoka wenye majina makubwa sana na mara nyingi amekuwa akitumika kwenye matangazo akitangaza vinywaji pamoja video games.

Jezi yake ndio inaongozwa kwa kuuzwa, kwenye msururu wa maduka ya kuuza vifaa vya soka KAMO, huku ikitegemewa mauzo kupanda ikiwa tu atajiunga na klabu yenye umaarufu mkubwa kuliko zote duniani huko ASIA - Manchester United. Umaarufu wa Kagawa ambao kwa sasa upo sawa na wachezaji kama Yuto Nagamoto wa Inter pamoja na mshambuliaji wa CSKA Moscow Keisuke Honda.

Lakini tofauti na wenzake Nagamoto na Honda ambao wanapenda sana kutokea kwenye vyombo vya habari, Kagawa yeye ni kama Paul Scholes hapendi mambo ya kuwa karibu sana na media kwa aibu aliyonayo.

Pamoja na kuwa na miaka miwili Ujerumani, bado anaongea aidha kupitia mtafsiri wake au vyombo vya habari vya Japan ambavyo vimekuwa vikimfuata.

Ikiwa atahamia England itabidi ajipange sana ama aendelee kuufuata mfano wa Paul Scholes ili aweze kuepukana na vyombo vya habari vya nchi hiyo ambavyo vingine vimeanza kusema United wanamsajili Mjapan huyo kwa sababu za kibiashara - kuongeza mauzo ya bidhaa zao barani Asia hasa nchini Japan. Lakini  ama kwa hakika huyu ni aina ya kiungo mshambuliaji ambaye United wanamhitaji ili kuweza kukirudishia kikosi uwezo wa kutawala tena soka la England.

Ndani ya misimu miwili aliyokaa na Dortmund - amesaidia klabu hiyo kuupora utawala wa soka la Ujerumani kutoka kwa Bayern Munich kwa mara mbili mfululizo.

SIENDI POPOTE-GYAN

 

Gyan
Asamoah Gyan
Mshambuliaji wa Sunderland Asamoah Gyan ametupilia mbali taarifa zinazosema anahama, akisema hana mpango wa kuondoka.
"Siondoki Sunderland, sibabaishwi na uvumi uliozagaa katika magazeti na tovuti," amesema Gyan akizungumza na tovuti ya MTNFootball.com.
Gyan kutoka Ghana, alifunga magoli 11 katika msimu wake wa kwanza katika ligi ya England.
"Nimejitolea kuichezea Sunderland kwa sababu napenda klabu na utamaduni wake," amesema Gyan.
"Nitabakia Sunderland msimu ujao, na katika siku zijazo, na nasubiri kwa hamu kukutana na wachezaji wenzangu na mashabiki wa Sunderland, tutakaporejea mwezi ujao."
Gyan ni mchezaji wa bei ghali zaidi kununuliwa na Sunderland, akitokea klabu ya Rennes ya Ufaransa kwa kitita cha zaidi ya pauni milioni 13, mwezi Agosti mwaka 2010.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25 amekuwa kipenzi cha mashabiki wa Sunderland, kutokana na mtindo wake na ufungaji wa magoli muhimu, likiwemo goli la kusawazisha katika dakika za majeruhi dhidi ya Newcastle mwezi Januari 2011.

SOUTH SUDAN JOINS FIFA 10 MONTHS AFTER INDEPENDENCE

South Sudan's football team

LLYOD NCHUNGA ABWGA MANYANGA YANGA

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI KUHUSU KUJIUZULU NAFASI YA UENYEKITI WA KLAB YA YANGA.
Ndugu wana Habari, najua kwamba taarifa hii itawafedhehesha wajumbe na wanayanga wanaotuunga mkono,hasa ukizingatia maamuzi ya pamoja ya vikao vyetu vya kamati ya utendaji vilivyopita kwamba hakuna wa kujiuzulu kati yetu mpaka tujue hatma ya mkutano mkuu ambao tulipanga ufanyike tarehe 15 Julai 2012, ukiachia mbali shinikizo la kujiuzulu linalotolewa na baadhi ya wazee na wanaojiita vijana wa klab, kwa wajumbe wa kamati ya utendaji, na hasa mimi kama mwenyekiti.
Nawashukuru wajumbe kwamba tulifanya kazi kwa pamoja na kwa ushirikiano mzuri, na hata pale tulipotofautiana tulifanya hivyo kwa hoja na kufikia maazimio ambayo wote tulikuwa tunawajibika nayo.
Tangu tumeingia madarakani tumeweza kushirikiana na kupata mataji matatu katika kipindi cha mwaka mmoja, yaani; Ngao ya Hisani 2010, Ubingwa wa ligi kuu ya Vodacom 2010/2011, na Ubingwa wa  Afrika Mashariki na Kati (Kagame Cup), 2011. Zaidi ni kwamba tuliuwa uteja kwa watani wetu wa jadi kila tulipokutana katika ligi ukiachia mbali mechi ya tarehe 6 Mei 2012, ambayo tulifungwa goli 5 bila, na kuleta mtafaruku mkubwa katika klab yetu.
Hali kadhalika tumeshirikiana  mpaka tumeweza kuboresha mkataba kati yetu na TBL kupitia Kilimanjaro Premium Lager, tumeingia mkataba na  kampuni ya NEDCO  kuendeleza mali zetu katika mtaa wa mafia na uwanja wetu wa KAUNDA baada ya kufikia hatua nzuri katika kupata hati miliki za maeneo yote mawili. Nafahamu kwamba kampuni hiyo iko katika hatua za mwisho za kumalizia michoro.
Hali kadhalika tuliingia mkataba wa kuzalisha na kuuza bidhaa zenye nembo yetu na hasa baada ya kufanya marekebisho yatokanayo na matakwa ya sheria kule BRELA na pia mkataba na kampuni ya NEXUS LTD, ambayo itakuwa inatutafutia wadhamini wa nje na ndani, kufanya promosheni zetu na kampeni kwa njia ya electronic kupitia mitandao mbalimbali na kukusanya data za wanachama na kusajili  wapya tukiwa na malengo ya kukusanya shilingi 300,000,000/= hadi 800,000,000/= kwa mwaka katika kipindi cha miaka mitatu. Haya yote tuliyafanya tukilenga kujitegemea kujazia mapengo yaliyokuwa yakitokana na kutegemea ufadhili wa mtu mmoja mmoja.
Kwa ridhaa yenu tumekua tukiendelea na mazungumzo na makampuni mbali mbali kwa ajili ya udhamini na kwa sababu maalum, nitazitaja katika hati ya makabidhiano kwa kiongozi ajaye.
Aidha, tumeshirikiana katika kufanya mambo mbali mbali ya kijamii, ikiwa ni pamoja na sikukuu ya kuadhimisha miaka 77 ya Yanga, sikukuu za pasaka, kuchangia jamii na waliokumbwa na maafa, na kongamano la vijana lililolenga kuwaamsha vijana kuitambua nafasi yao katika Yanga ikiwa ni pamoja na kupata azimio la kuanzisha SACCOSS ya Yanga, ambapo maombi yapo kwa msajili Manispaa ya Ilala.
Haya yote nayataja ikiwa ni kuwashukuru kwa ushirikiano na ikiwezekana muweze kuyakamilisha yaliyobaki ambayo mtaona yalikuwa mazuri.
Lakini pia tulipopata matatizo tulikuwa pamoja.  Nichelee kusema tu kwamba tulisimama pamoja baada ya kujiuzulu Makamu Mwenyekiti wetu Ndugu Davis Mosha na mjumbe wetu  ndugu Seif A. Seif, Ali Mayayi, na wengineo, kwani tulifungwa na katiba.Tulisimama pamoja pia katika suala la kujiuzulu ndugu Yusuf M. Manji, aliyekuwa mdhamini mteule na mfadhili mkuu ambaye sasa ameonyesha nia ya kurudi nanyi mkaridhia mkutane naye. Awali, tulitumia kila jitihada za kumrejesha lakini ikashindikana.
Hata hivyo doa limetupata baada ya kufungwa na watani wetu goli 5 bila, ambapo kuna wanachama wanaoelewa na wasioelewa kabisa.
Ninachokiona mimi ni usaliti wa hali ya juu uliombatana na matukio mbalimbali yaliyopita na yanayoendelea hadi kujaribu kupindua uongozi wa halali wa kidemokrasia. SIWATUHUMU WACHEZAJI MOJA KWA MOJA, isipokuwa  mfululizo wa matukio wiki tatu kabla ya mchezo ule na sasa, inaonyesha kwamba kulikuwa na usaliti mkubwa ambao sisi hatukuweza kuubaini mapema.
Sioni mantiki katika hoja kwamba wachezaji walikuwa wakidai mishahara, posho n.k.  Au ati mtendaji wetu alishikiliwa Arusha kwa deni la hoteli, ndiyo  tuvune bao 5!
Kwa wanaoijua Yanga, imewahi kuwa na madeni makubwa katika Hoteli mbali mbali, mawakala wa ndege n.k, na baadhi tumeyakuta na sisi tumekuja tukayalipa. Hii imewahi kutokea kabla na wakati akiwepo mfadhili, sembuse sisi tulioachwa baki, na bado wachezaji walicheza kwa morali.
Hata hivyo, utamaduni wa kutimuana baada ya matokeo mabaya ni dhambi ambayo itatula kama hatutaiacha, kwani wenye hila na uchu wa madaraka wataendelea kutumia mbinu hiyo ili kuuondoa uongozi wa kidemokrasia.
Baada ya mapinduzi kushindikana na TFF kuonya kuhusu mapinduzi hayo, wazee kupitia msemaji wao , Mzee Akilimali wamesikika katika kipindi cha Michezo  cha Redio moja maarufu hapa nchini wakidai kwamba ni bora Yanga ishushwe daraja au kufungiwa kuliko mimi kuendelea kuongoza!
Hii imenikumbusha HEKMA ZA MFALME SELEMANI akiamulia ugomvi wa wanawake wawili waliokuwa wakigombea mtoto naye akaamuru wamgawane nusu kwa nusu. Yule mwenye mtoto kweli alimuomba Mfalme amuachie mwenzie kuliko kumkata nusu.
Kwa hekma hiyo nimeamua kujiuzulu nafasi yangu katika Uenyekiti  wa Yanga kwani ni klab ninayoipenda hata kama sio kiongozi kwa mujibu wa ibara ya 28 ya katiba yetu.
Vile vile siko tayari kuona klab yangu ikisalitiwa au kuhujumiwa eti kwa sababu tu mimi ni kiongozi.
Natumaini kamati ya utendaji kwa pamoja na wale tuliowateua chini ya ibara ya 29(3) ya katiba ya Yanga pamoja na bodi ya wadhamini, itawaongoza wanachama mpaka kufikia mkutano mkuu kwa  mafanikio zaidi.
 Nitaendelea kuwa mwanachama mwadilifu na nitatoa mchango wangu wa hali na mali pale nitakapo hitajika na nikiwa  na uwezo wa kufanya hivyo.
YANGA DAIMA MBELE, NYUMA MWIKO.
Wasalaam,


LLOYD NCHUNGA BIHARAGU.

Nakala kwa:-
Mama Fatma Karume,Mdhamini
Francis Kifukwe, Mdhamini
Bwana Yusuf Manji – Kwa taarifa

SEPP BLATTER: MIKWAJU YA PENALT INAPOTEZA MAANA YA SOKA

TFF: HATUTOMLIPA HATA SENTI MOJA JAN POULSEN

SHIRIKISHO la Soka Tanzania(TFF) limeweka wazi kwamba aliyekuwa kocha wa timu ya taifa(Taifa Stars)Mdenmark Jan Poulsen hatalipwa mishahara yake ya miezi mitatu iliyosalia katika mkataba wake.

Msimamo huo wa TFF umekuja baada ya  gazeti la Mwananchi wiki iliyopita kumkariri Poulsen akililalamikia shirikisho hilo lwa kutolipwa mshahara wake wa mwezi mmoja,sambamba na fidia inayotokana na kuvunjwa kwa mkataba wake.
Hivi karibuni TFF ilisitisha huduma ya Poulsen kwa Taifa Stars na badala yake ikamtangaza aliyekuwa kocha wa timu za taifa za vijana, Kim Poulsen kuchukua jukumu hilo.

Akizungumza na Mwananchi, Ofisa Habari wa TFF, Boniface Wambura alisema kuwa hatua ya kutomlipa Poulsen mishahara ya miezi mitatu inatokana ukweli kwamba kocha huyo hatakuwa na kazi ya kufanya katika kipindi hicho cha miezi mitatu ya mkataba wake kilichosalia hadi Julai 30.

"Kwanza kabisa ieweweke kwamba serikali ndiyo iliyokuwa inamlipa  Poulsen mshahara baada ya kuingia naye mkataba na sio TFF."Katika utaratibu wa kawaida wa serikali tunaoufahamu awezi kulipwa mshahara wa bure wakati hajafanya kazi yoyote,huo ndio ukwli wenyewe,"alisema Wambura

Akifafanua zaidi, Wambura alisema TFF iliamua kusitisha huduma za Poulsen licha ya kwamba mkataba wake unaendelea kuwa hai kwa lengo la kuta nafasi kwa kocha mpya kupanga mipango ya muda mrefu.

"Kila baada ya muda fulani kocha anatakiwa awasilishe ripoti ya timu yake,sasa utapataje ripoti sahihi wakati kesho kutwa mkataba wake unamalizika.

"Pia niweke vizuri hapo,TFF haikuvunja mkataba wa Poulsen bado upo na utamalizika Julai 30 tulichokifanya ni kuzungumza nae na kukubaliana kwamba hakutaongeza mkataba hivyo tunatafuta kocha mwingine,"alisema.

Wambura aliongeza kuwa,licha ya kibarua cha kocha huyo cha kuinoa Taifa Stars kusitishwa,bado TFF itaendelea kuwa nae katika mkataba mwingine unaohusiana na ukufunzi wa makocha nchini.

"Poulsen pia alikuwa na kazi nyingine ya ukufunzi wa makocha hata hapa ametuaga anakwenda kwao kuhudhuria harusi ya mtoto wake akirudi ataendelea,"alisema Wambura

Kwa  upande mwingine kusitishwa kwa kibarua cha Poulsen kunahusishwa  na shinikizo la wadau wa soka waliotaka mabadiliko katika benchi la ufundi kufuatia Taifa Stars  kuporomoka mfululizo kwa takribani miezi saba kwenye viwango vya ubora vya Shiriki

BOBAN NA SAMATA KUONGOZA MASHAMBULIZI TAIFA STAZ

KOCHA wa timu ya Taifa 'Taifa Stars', Kim Poulsen amewapa majukumu ya ufungaji mabao kiungo mshambuliaji, Haruna Moshi 'Boban' na mshambuliaji Mbwana Samata katika kikosi chake kilicho kambini hivi sasa.

Katika mazoezi ya kikosi hicho yanayoendelea kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, Kim amekuwa akiwachezesha pamoja Boban anayeichezea Simba na Samata anayekipiga katika klabu ya TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) na kuonyesha maelewano makubwa na wakupachika mabao mengi ya kiufundi.

Kim amekuwa akikigawa kikosi chake katika timu mbili na kuwachezesha pamoja, Samata anayetumika kama mshambuliaji namba tisa na Boban anayetumika kama mshambuliaji namba 10.

Kitendo cha Kim, kumtumia Boban kama mshambuliaji badala ya kiungo kama asili yake, kimeonekana kuwa na faida, kwani kimetoa fursa kwa chipukizi wa JKT Ruvu,  Frank Domayo kutumika kama mpishi namba nane.

Naye Mrisho Ngasa ambaye amekuwa akimtumia kama winga wa kushoto kama ilivyo kwa Mwinyi Kazimoto anayecheza winga wa kulia, mara kadhaa amekwaruzana na Kim kutokana na tabia yake ya kung'ang'ania kukaa pembeni badala ya kuingia ndani kuwasaidia viungo Domayo na Shaabani Nditi hasa pale mashambulizi yanapoelekezwa kwao.

Katika safu ya ulinzi, kocha huyo Mdenmark amekuwa akimpanga Aggrey Morris kama mlinzi wa kati akisaidiana na Kelvin Yondan anayecheza namba nne huku Shomari Kapombe akiimarisha ulinzi wa kulia kama ilivyo kwa Waziri Salum anayedhibiti nafasi ya beki wa kushoto.

Picha halisi ya kikosi cha kwanza cha Kim kutokana na mazoezi hayo ni kipa Juma Kaseja, Shomari Kapombe,Wazir Salum, Kelvin Yondan, Aggrey Morris, Shaaban Nditi, Mwinyi Kazimoto, Frank Domayo, Haruna Moshi'Boban', Mbwana Samata na Mrisho Ngasa.

Wakati huo huo, timu ya Taifa ya Malawi (The Flames) inatarajiwa kutua leo saa 10 jioni kwa ndege ya Air Malawi tayari kwa kuivaa Taifa Stars kesho katika pambano la kimataifa la kirafiki litakalopigwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Taifa Stars itaikabili The Flames ikiwa ni maandalizi ya mechi yake ya kuwania kufuzu kushiriki Fainali za Kombe la Dunia Kanda ya Afrika dhidi ya Ivory Coast itakayofanyika Juni 2 mwaka huu jijini Abidjan, huku pia Malawi ikitumia mechi hiyo kujiandaa kupambana na Kenya.

Viingilio katika mtanange wa Taifa Stars na Malawi  vitakuwa Sh 3,000 kwa viti vya bluu na kijani, Sh 5,000 kwa viti vya rangi ya chungwa, Sh 15,000 kwa jukwaa la viti maalumu B na C na Sh 20,000 kwa jukwaa la viti maalumu A.

Wednesday, May 9, 2012

DALGLISH PLEASED WITH A SEASON

Liverpool manager Kenny Dalglish felt his first full season back in charge of the Anfield club would be defined as successful after the 4-1 thrashing of Chelsea.
The Reds underperformed in the league, with victory over the Blues only their sixth at home all season, but the club have also won the Carling Cup and finished runners-up in the FA Cup.
But after losing out to the Londonders at Wembley last weekend, Dalglish took a number of positives from the penultimate match of the season.
"We've got a bit of silverware back in the cupboard after six years, we're back in Europe at the first time of asking, we were near to winning the FA Cup final. Not a bad first season," he said.
"The players understand better than everyone the club's expectations and they're probably more educated than most.
"I think the players will be happy to finish on a high at Anfield. That performance was on a par with a lot of other performances where we've not had the result. Tonight we got that.
"For us it was a satisfying evening

Tuesday, May 8, 2012

WACHEZAJI AZAM WAPONGEZWA

Mwenyekiti wa Azam FC Abubakara Bakhresa amewapongeza wachezaji na viongozi wa Azam FC kwa kukamilisha dhamira hiyo pamoja na kuridhishwa na mafanikio ya klabu yake.
“nimefurahi na kuridhishwa na mafanikio ya klabu, ndani ya misimu minne, msimu wa kwanza tulikuwa tunajilinda tusishuke daraja lakini kwa kipindi hiki tumeweza kuwa katika nafasi ya pili ni mafanikio makubwa kwetu” alisema Bakhresa.
Mwenyekiti alijivunia juhudi na nidhamu imechangia kuifikisha timu katika mafanikio hayo kwa kuwa wachezaji wameonyesha nidhamu kubwa na wale walioenda kinyume walichukuliwa hatua.
Akizungumzia changamoto waliyokutana nayo msimu huu Bakhresa alisema klabu ilisimama kidete kupambana na kila hila iliyokuwa inatengenezwa makusudi kuharibu jina la Azam FC kwa kutumia mbinu mbalimbali ikiwemo kuharibu mechi ili kuishushia heshima klabu.
Alisema kuwa na umoja kati ya viongozi na juhudi za wachezaji wameweza kupambana na hali hiyo hadi mwisho ambapo timu imekamilisha lengo lake kwa kufanya vizuri katika mechi zake.
Akielezea muenendo wa soka nchini, alisema kipindi cha sasa soka linakua na kutoa ajira kwa wachezaji alitolea mfano kwa Azam FC wameweza kuwapa mahitaji muhimu ambayo pengine si rahisi kuyapata katika vilabu vya nje ya nchi.
“Azam FC inanufaika na kutoa ajira kwa vijana kupitia michezo na wachezaji wananufaika kwa kuichezea Azam FC” alisisitiza Bakhresa.
Mbali na mafanikio Mwenyekiti alimpongeza mshambuliaji wa klabu hiyo John Bocco kwa kumaliza ligi akiwa mfungaji bora na mchezaji bora wa klabu hiyo na kuvunja rekodi kwa kufikisha magoli 19.
Alisema mafanikio ya Bocco yamechangiwa na timu nzima, bila kuwa na wachezaji wengine asingekuwa katika nafasi hiyo aliwapongeza na kuwashukuru wachezaji kwa kufanikisha mafanikio ya Bocco.
Amefurahishwa na kuutekelezaji wa mapema uliofanywa na klabu hiyo ambao ni kuwa na kituo cha mazoezi 'Training centre' chenye uwanja wa kisasa, gym yenye kiwango cha hali ya juu pamoja na hostel za kisasa ambazo zinatumiwa na timu ya vijana (Azam Academy), na kutwaa ubingwa wa kombe la Mapinduzi 2012.
Alisema hayo ni sehemu ya mipango ya klabu ya kuleta mapinduzi ya sika nchini na kauhidi kuwa timu itaendalea kwa kufanya vizuri katika ligi ijayo pamoja na mashindano ya kimataifa.
Mwenyekiti ametangaza rasmi dhamira ya msimu ujao ni kutwaa ubingwa wa ligi kuu ya Vodacom, kufanya katika michezo ya kimataifa ya Kombe la Shirikisho Afrika na kombe la Afrika Mashariki na Kati 'CECAFA'.
Amewaaga wachezaji kwa kuwatakia mafanikio mema wakat huu wa likizo, watumie vema likizo zao kwa kulinda vipaji hivyo na kuwatakia maisha mema wachezaji watakaoachwa na timu hiyo.
Aliwashukuru wote waliohusika kuifikisha timu katika hatua hiyo na kutambua mchango wa waandishi wa habari za michezo nchini kwa kuwapa vyeti vya shukrani.
Hafla ilihuduriwa na viongozi wa Shirikisho la Mpira nchini TFF, wawakilishi wa vilabu vya ligi kuu, Mbunge wa Kinondoni, Iddi Azan na vyombo vya habari.
Azam FC iliingia ligi kuu misimu minne iliyopita, msimu wa kwanza 2008/09 ilimaliza ikiwa nafasi ya nane, msimu wa pili 2009/2010 na msimu wa tatu 2010/2011 timu ilimaliza ikiwa katika nafasi ya tatu na msimu huu 2011/2012 imemaliza msimu ikiwa nafasi ya pili.

ASSOU-EKOTTO MULLS EXIT

Benoit Assou-Ekotto admits he may be tempted to leave Tottenham by the promise of more money and regular Champions League football.
The 28-year-old has established himself as a key part of the Spurs squad since his arrival from Lens in a £3.5m deal in 2009.
However, the Cameroon international insists he is always open to new challenges and could quit White Hart Lane if a decent offer arises in the summer.
"Everything is possible," he told France Football. "When I met the chairman last January he told me that, if a club bigger than Tottenham came in for me, he wouldn't necessarily be against my departure.
"If there is a change at Tottenham - some more money is made available - I wouldn't be against the idea of staying, but otherwise I'll try to move forwards, as I did when I left Lens.
"All players want to play in the Champions League. A few months ago, I said I never wanted to play in the Europa League because that competition is useless.
"I have a gentleman's agreement with the chairman. As he is a man of his word, I hope that will make things easier if a great club comes in."

LIVERPOOL VS CHELSEA LIVE

Former Kop idol Fernando Torres returned to Anfield for the first time since his £50m departure in January last year as one of eight changes for Chelsea.
With his team the outsiders to finish in the top four, manager Roberto di Matteo made numerous alterations to the team which won the FA Cup against the Reds on Saturday as this month's Champions League final against Bayern Munich is his primary focus.
Liverpool made four changes from their team, with captain Steven Gerrard absent from the squad but Wembley goalscorer Andy Carroll returning to the line-up.
The teams are in for tonight's Sky Live FA Cup final rematch at Anfield. Follow the encounter blow-by-blow here from 2000 or on Sky Sports HD2 and Skygo.
Liverpool: Reina, Johnson, Carragher, Skrtel, Agger, Shelvey, Henderson, Rodriguez, Downing, Suarez, Carroll
Subs: Doni, Coates, Kuyt, Spearing, Sterling, Kelly, Bellamy.
Chelsea: Turnbull; Ferreira, Ivanovic, Terry, Bertrand; Essien, Romeu, Malauda; Ramires, Torres, Sturridge.
Subs: Hilario, Cole, Lampard, Mata, Lukaku, Kalou, Hutchinson.
Referee: Kevin Friend (Leicestershire

EVRA: OUR EMPIRE WILL SURVIVE

Skipper Patrice Evra insists losing the Premier League title will not spell the end of the Manchester United empire.
Manchester City are on the brink of winning their first top-flight crown since 1968 - victory over QPR at the Etihad next week will confirm it.
But Evra has warned their local rivals that City's first title in 44 years does not mean the end of an era at Old Trafford.
"I know that if we don't win the league then a lot of people will say this is the end of the empire and ask how we will survive," said the France full-back.
"But there is a lot of talent at this club.
"We've had to deal with a lot through injuries and losing experienced players last summer and it's never easy to find a solution immediately."
Midfielder Michael Carrick believes QPR might just cause a huge upset.
"You can't hide from it," he said. "We kept believing and we still believe anything can happen. It's not over.
"We can still hope. We still have to get a win at Sunderland, which is not a given. Then all we can do is hope QPR do what they've got to do and help us out.
"We're still in it and still have a fighting chance.

SAGNA BLAME JOHNSON FOR BREAK

Arsenal full-back Bacary Sagna has accused Norwich midfielder Bradley Johnson of deliberately contributing to his broken leg.
The France international has been ruled out of this summer's European Championships after collapsing in the first half of Arsenal's 3-3 draw with the Canaries.
The injury occurred shortly after Johnson had stood Sagna's leg, the same one he broke earlier in the season, and the 29-year-old believes there was intent from the City midfielder.
"I think he did it on purpose," Sagna told sports daily L'Equipe on Sunday. "He stepped on my leg. Play continues, I get back on my feet. And when I tried to control the ball, I felt a crack, just like the first time at Tottenham.
"He stepped right where the plate was. I think the plate pressured (the bone). It's a neat break, just above the plate.
"That's how it is. It's football

CHELSEA CONFIRM NEW YORK DATE

Chelsea will take on Carlo Ancelotti's Paris Saint Germain in New York this summer.
The game, which takes place on July 22, will be the first football match played at the new Yankee Stadium and will be the first time Ancelotti has faced the club he won the double with.
The Blues will then face AC Milan at the Sun Life Stadium in Miami on Saturday, July 28.
Chelsea had previously confirmed matches against Seattle Sounders on July 18 and Philadelphia on July 25.
Chelsea have not played in New York City since the summer of 1954, and chief executive Ron Gourlay told the club website: "We are very excited to announce these two final fixtures in our summer tour.
"Chelsea Football Club is delighted to be heading to New York after such a long time away, and it will be a real pleasure to visit Yankee Stadium for what is sure to be a competitive game.
'Paris St Germain represents a true test for us in our preparations for the new season. We know Carlo well and respect the superb job he did for us, and continues to do in France. It should be a fantastic game.
'Southern Florida is a hotbed

FERGASON LEMENTS DEFENSIVE SLIPS

Sir Alex Ferguson believes Manchester United could be sitting at the top of the table had he taken a leaf out of Roberto Mancini's management manual.
Mancini's Manchester City side are currently in pole position to claim the Premier League title, leading United by goal difference going into the final game of the season.
And after watching City close out a 1-0 win against his side last weekend, Ferguson believes had he employed similar tactics against Everton, United may not have twice thrown away a lead to drop two points in the 4-4 draw with the Toffees.
"In the end we just ran out of time, as Mancini made changes to give him five at the back," said Ferguson. "It's the Italian mentality - and maybe we should sometimes go down that road.
"We could certainly have done with bolting up the game against Everton. If we had done just a fraction of what City did, I would probably be saying quite a different thing.
"It is not in our nature to put up the shutters and I like to think that it is our attacking, adventurous approach that has made United famous.
"On balance it's a policy that has also served us well in terms of trophies. But if we lose the league this year there is no doubt the pivotal match was the 4

MADRID WANT PAPISS DEMBA CISSE

Real Madrid scouts have been watching Papiss Demba Cisse with a view to making a move for the Newcastle United this summer - THE TIMES

PEP REJECT OFFER FROM CHELSEA

 

Pep Guardiola has rejected a £12m-a-year offer from Chelsea - which could open the door for Roberto Di Matteo to land the manager's job permanently

BREAKING NEWSS!!!!!!!!

Tegete avalishwa jezi ya simba na washabiki wa simba baada ya mechi ya simba na yanga kumalizika

MILOVAN ANUNUA BEKI

KOCHA wa Simba, Milovan Cirkovic, amepanga kufanya marekebisho kwenye safu ya ulinzi kwa kusajili mabeki imara zaidi.

Milovan ambaye timu yake iliichapa Yanga mabao 5-0 juzi Jumapili sambamba na kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara, alisema kuwa nafasi nyingine hana matatizo nazo ingawa anafikiria pia kuzigusa.

"Kwa sasa nitafanya mabadiliko kidogo kwenye safu ya ulinzi kwa kuongeza nguvu zaidi. Hiyo ndiyo sehemu ambayo imekuwa na matatizo kwenye mechi zetu," alisema.

"Nitaimarisha zaidi beki, nahitaji timu imara zaidi, hizo idara nyingine nitafanya tathmini ya kina na ninaweza kuzigusa kidogo, lakini hazina matatizo sana kama kwenye ulinzi."

Kwa sasa Milovan anaiandaa timu yake kwa ajili ya mechi ya marudiano ya Kombe la Shirikisho dhidi ya Al Ahly Shandy itakayofanyika Ijumaa huko Sudan.

Katika mechi ya awali Simba ilishinda mabao 3-0 jijini Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa duru za ndani za Simba, Milovan atamtema beki wa Uganda, Derrick Walulya na pengo lake kuzibwa na beki mwingine wa kigeni.
Tayari Simba imemsajili kiungo wa Uganda, Mussa Mudde.

PAPIC AMPELEKA OKWI ULAYA

Papic: Kocha (Minziro) aliyekuwa na Yanga kambini anajua vizuri zaidi, amekuwa na wachezaji kwa siku zote kwa hiyo alijua alichokifanya. Mimi sikuwa na kibali cha kufanya kazi. Hilo nadhani kocha aliyekuwapo anajua zaidi.

Mwanaspoti: Unadhani nani alikuwa mchezaji bora wa mechi?
Papic: Hilo halina ubishi Okwi. Amesababisha mabao yote matano.

Mwanaspoti: Unadhani anaweza kucheza Afrika Kusini au Ulaya?
Papic: Aende Ulaya, soka lake ni kubwa, tatizo jingine ni kuwa akienda Afrika Kusini ni ngumu kwenda Ulaya, ila akienda Ulaya anaweza kuanza na timu ndogo baadaye akapata timu kubwa.

Mwanaspoti: Vipi mwamuzi wa mchezo?
Papic: Alichezesha vizuri sana. Yanga imefungwa mabao matano, lakini hakuna sehemu unaweza kumlaumu mwamuzi. Alifanya kazi nzuri.

Mwanaspoti: Ungekuwa benchi la Yanga ungeweza kubadilisha matokeo?

Papic: Swali zuri, lakini siwezi kukujibu. Mkataba wangu umekwisha na Yanga. Ila kila kitu kingekuwa kizuri kama wachezaji wangekuwa wanalipwa mishahara yao na kocha angekuwa analipwa na kutafutiwa kibali cha kazi.
Mwanaspoti: Unashauri Yanga wafanye usajili wa nafasi zipi?

Papic: Siwezi kutoa ushauri, sasa nafikiria kujiunga na timu nyingine. Lakini Yanga ina matatizo mengi.
Mwanaspoti: Unajiunga na timu gani?
Papic: Siwezi kusema hapa, pengine unajua.

SIMBA YAMFUNGA YANGA 5-0

Simba imemfunga yanga 5-0 magoli yaliyofungwa na okwi 2, sunzu 1, mafisango 1 na kaseja goli moja. Yanga wlitawla mchezo kipindi cha kwanza na Simba walitawala kipindi cha pili

Monday, April 30, 2012

SIMBA HOYEEEEEEEE!!!!!!

Simba sport club wawakilishi pekeee wa michuano ya kimataifa jana wamefanikiwa kuifunga Alh Shand mabao 3-0. mabao hayo yamefungw na Haruna Moshi Boban, Mafisango na Emmanuel Okwi. Kikosi kilichoanza jana ni Juma Kaseja, Amiri Maftar, Kapombe, Cholo, Yondani, Mafisango, Kazimoto, Uhuru Sulemani, Okwi, Boban na Sunzu.